Tanzania emblem

Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Afrika

Urithi wa Ukombozi, Fahari ya Afrika

Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Afrika

Malengo

LENGO KUU

  • Kukusanya, kuweka kumbukumbu, kuhifadhi na kuendeleza historia ya ukombozi wa Afrika iliyotokana na harakati za kupigania uhuru.

MALENGO MAHSUSI

  • Kuamsha na kuendeleza utafiti wa urithi wa ukombozi wa Afrika;
  • Kulinda, kuhifadhi na kuendeleza Urithi wa Ukombozi wa Afrika;
  • Kuanzisha mfumo wa kuenzi mashujaa na kuendeleza umiliki wa urithi wa ukombozi wa Afrika;
  • Kujenga uwezo wa kitaalamu katika kusimamia na kueneza urithi wa ukombozi wa Afrika;
  • Kuratibu Programu hii kwa ushirikiano miongoni mwa Nchi Wanachama wa Programu hii; na
  • Kutangaza maeneo ya urithi wa ukombozi katika gazeti la Serikali ili yalindwe kisheria.